WATUMISHI HOUSING KUPITIA FAIDA FUND KUFANYA MKUTANO WAKE WA MWAKA AGOSTI 10 MWAKA HUU

Shirika la Watumishi housing (WHI) likishirikiana na Bank ya CRDB, kwa pamoja wameandaa, Mkutano mkuu wa Kwanza WA mwaka wa mfuko WA uwekezaji WA farida FAIDA FUND ambao utafanyika AGOSTI 10 mwaka huu Jijini Dar ar es Salaam.

Akizungumza na waaandishi wa habari hii Leo AGOSTI 6 2024, Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi housing WHI, Fred Msema amesema.

Mkutano huo utafanyika kwa kuzingatia Sheria ya mamlaka ya masoko na Miraji (CMSA) ambapo kila mwaka WHI itakuwa ikiandaa mkutano huo, ili kutoa fursa kwa wanachama wao KUJADILI maswala mbalimbali yanayohusu mfuko pamoja na kupokea taarifa zenye maslahi kwa wawekezaji.

Aidha Msemwa amesema tangy kuanzishwa kwa mfuko WA faida ambao unalenga kutoa  fursa wawekezaji wote WA mfuko kupokea na KUJADILI taarifa ya fedha ya mfuko kwa kipindi cha mwaka unaoishia juni 30 2023.

Katika hatua nyingine Msemwa Ameongeza kuwa katika kipindi cha muda mfupi mfuko wa (WHI) kupitia faida fund umeweza kuweka misingi imara utakaoweza kuziba ombwe la wawekezaji wadogo kushindwa kushiriki kwenye uwekezaji katika masoko fedha.

Akitaja faida na sifa za mfuko WA faida ambapo amesema mfuko huo ndio WA Kwanza Nchini kushusha kianzio cha kuweka kwa angalau kiasi cha Shilingi elf kumi 10000 Kwa kuanzia na wawekezaji wote iwe wadogo au wakubwa.

Vilevile amesema mfuko wao ndio mfuko pekee mwekezaji anaweza kuwekeza na kupata faida na kuchukua fedha zake bila kujaza fomu yoyote au kufika ofisini.


Naye Meneja Biashara Kutoka Bank ya CRDB, ambaye pia ndio wasimamizi na Muangalizi wa Mfuko huo.

Bi Mary Mponda ametumia fursa hiyo kuwataka Wananchi na wawekezaji kwa ujumla kuweendelea kutumia mfuko WA faida fund kuwekeza lakini pia kuwakaribisha wadau wote kupitia Watumishi housing kushiriki mkutano huo wa mwaka na amewaondoa hofu kuhusu Amana na fedha zao kuwa zipo salama.

Powered by Blogger.