SAMIA KUZINDUA SGR DAR HADI DODOMA AGOSTI MOSI

Waziri wa Ujenzi na uchukuzi Mh Makame mbalawa amesema Serikali ipo tayari kuanza kutoa huduma ya usafirishaji abiria na mizigo kwa kiwango cha Kimataifa kupitia Treni ya Viwango SGR.


Aidha mbarawa amesema kuanzia sasa Serikali itaanza Huduma ya Usafiri katika Reli ya Kiwango cha Kimataifa, kutasaidia kwa kiwango kikubwa ongezeko la Mapato kwa Taifa pamoja na Maendeleo ya shughuli za Kiuchumi.

Shughuli nyingine ambazo zitaongezeka Kipato ni zile za Kijamii na Kiutawala, kwani SGR inatoa Usafiri wa uhakika na haraka.

Taasisi binafsi na za umma kuwekeza kwenye treni ziwekeze kwenye Miundombinu ya Reli ambayo Serikali imewekeza ili kufungua milango ya kibiashara Sambamba na kuifunga bandari ya dar es salaam ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa tegemeo kwa nchi jirani ea Tanzania.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania-TRC-MASANJA KADOGOSA amesema Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imewawezesha kwa vitendea kazi, huku akiwahakikishia wananchi kwamba yapo Mabehewa ya kutosha.
Treni hiyo itakua na uwezo wa kubeba Mizigo hadi inayofikia Tani Elfu 10 kwa mpigo ambayo ni sawa na Malori Mia 5.



 

Powered by Blogger.