WANANCHI NYEBURU: WALIA NA SERIKALI UBOVU WA BARABARA UKOSEFU MAJI SAFI

Na Jumanne magazi 

29.03.2026

Dar es salaam 

Serikali imesema  inaandaa mpango kazi utakao boresha miundombinu ya barabara pamoja na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa kata  ya Buyuni na viunga vyake, ikiwemo mtaa wa nyeburu A,na B iliyopo katika Jimbo la Ukonga jijini dar es salaam.

Akizungumza na Wananchi kwenye mkutano wa hadhara, Afisa Tarafa wa Ukonga, Bw Kheri William, amesema serikali imepokea kilio na maombi ya Wananchi wa Mtaa wa Nyeburu kwa niaba ya wenzao wa Jimbo lote la ukonga, na kwenda kutatua changamoto kaubwa ya barabara pamoja na kuondoa kero ya muda mrefu ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ndani ya Mtaa wa Nyeburu,pamoja na kata nzima ya buyuni.

Kheri amesema ni kweli Hali ya miundombinu ya barabara kwenye mitaa mingi ndani ya kata ya buyuni ni mibovu hususani,mtaa wa Nyeburu A na B jambo ambalo huleta adha kubwa kwa wananchi,hususani kipindi hiki cha msimu wa Mvua unaoendelea, lakini pia ukosefu wa maji safi na salama.

Naye Mbunge wa Jimbo la ukonga Mheshimiwa Bakari Shingo, amewaasa Wananchi wa kata ya buyuni na mtaa wa Nyeburu kuwa wavumilivu na kuwaamini viongozi wao walio wachagua, wakati wanakwenda kushughulikia kero zao hizo, ambapo ameahidi kufikisha kilio chao kwa mawaziri wanaohusika, na sekta ya Maji na miundombinu.

Kuhusu Ukosefu wa maji safi na salama Mh mbunge pamoja na Diwani wa kata ya Buyuni MH Jesca Mahmoud msolla, wamefanya Mawasiliano ya moja kwa moja na  Mkurugenzi wa Dawasco, ambaye amekiri kuwepo kwa kero hiyo ya maji, ikiwemo kukwama kwa baadhi ya miradi ya usambazaji wa huduma hiyo, jambo ambalo ameahidi kulifanyia kazi kwa hatua stahiki kwa kipindi na muda wa miazi ijayo.


Kwa upande wake Diwani wa Buyuni,Mh Jesca msolla, ameishukuru serikali pamoja na Mh Mbunge, kukutana na Wananchi, wa kata hiyo, ili kuzitafutia ufumbuzi kero za wananchi hao, ambazo ni maji na barabara.

Ambapo amesema "viongozi  ni jukumu latu kuhakikisha wanatatua changamoto zote za wananchi wetu kwani wao ndio mabosi na waajili wetu amesema Mbunge huyo.

kikao hicho kimeazimia kuwa kuwa viongozi wanakwenda kushughulikia changamoto ya maji na barabara kabla ya kuja na majibu kwenye kikao kijacho.


Mapema kwenye mkutano huo mwenyekiti wa mtaa wa Nyeburu, Bw Sadati Athumani Rwetabula,aliiomba na kuishahuri Serikali kupitia taasisi zake ikiwemo Dawasco wakati ikisubiri miradi mikubwa ya muda mrefu kutekelezwa, kuchimba Visima vya dharula ambayo vitasaidia kupunguza makali ya ukosefu wa maji wananchi wa Nyeburu na viunga vyake.

Nao wananchi Zaituni Mohd Ali, Mohammed Omari Kitenge,wameupongeza uongozi wa serikali ya mtaa wa Nyeburu, hususani mwenyekiti na kamati tendaji yake,kuandaa mkutano huo muhimu uliowakutanisha wananchi na viongozi wa serikali akiwemo Afisa Tarafa kwani umeleta faraja kubwa kwa wananchi na wameomba kuwepo na utaratibu wa kufanya mikutano ya namna hiyo mara kwa mara

Powered by Blogger.