MUSLIM HASSANNALI: ACHUKUA FOMU JIMBO LA KINONDONI


Na Jumanne Magazi 

30.06.2025

Dar es salaam 

Muslimu Hassanali amejiweka rasmi kwenye kinyang’anyiro cha ubunge kwa kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania Jimbo la Kinondoni katika uchaguzi ujao

Muslimu alichukua fomu hiyo katika ofisi ya CCM Wilaya ya Kinondoni, mkoani Dar es salaam, mbele ya viongozi wa chama hicho
Muslim Hassanali anajiunga na orodha ya wanachama wa CCM wanaowania ridhaa ya kugombea ubunge kupitia chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu, huku Jimbo la Kinondoni likitarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na mvuto wake wa kisiasa
 

Powered by Blogger.