CCM:Hatuna historia ya kushindwa uchaguzi zb

Ma Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kutokana na   udhaifu  wa upinzani ,ukikabiliwa  na  ombwe la uongozi, hauwezi  kukishinda  CCM  chenye sera za  kimaendeleo  .

CCM kimesisistiza kushinda baada ya kutekeleza vyema ahadi  zake za kisera huku kikihimiza  Amani, Umoja na Upendo .

Hayo yameelezwa na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC  Idara ya Itkadi,Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto  Khamisi,  aliyesema  upinzani unapodai utashinda  ni  sawa na kuota ndoto  mchana .

Mbeto  alisema kwa utelelezaji mkubwa wa sera ambazo zimeleta  mabadiliko ya maendeleo  Zanzibar, hakuna mwananchi atakae upigia kura upinzani.

Alisema ikiwa viongozi wa ACT Wazalendo  wanaamini watashinda, matumaini hayo ni sawa  na kuisubiri treni ya SGR katika kituo cha daladala .

Mbeto alisema CCM kitapata  ushindi kutokana na mageuzi  ya kimaendeleo yaliofanyika  na baada ya  kuwahimiza wanachama  wake kujiandikisha  katika  Dafrari la Kudumu la Wapiga kura.

Mwenezi huyo alisema hata ASP  hakikuwa na historia  ya kushindwa kwani  chaguzi  zote tatu za mwaka 1957,1961 na 1963 , ASP  kilishinda ila wakoloni  hawakutoa madaraka.

Mbeto alisema hata  CCM   kimendelea kushinda toka   mwaka 1995 hadi 2020 na sasa kinajiandaa tena kushinda na kuunda dola . 

'Tutashinda kwa kufuata misingi ya demokrasia. CCM ni chama kinachotegemea uamuzi  wa walio  wengi . Tumemsimamisha mgombea urais anayetakiwa na wananchi, mchapakazi na kiongozi  mzalendo ' Alisisitiza.

Hata hivyo Mbeto  aliwahimiza wananchi, wafuasi ,wakereketwa  na mwnachama wa CCM, kujitoeza ili  kujindikishaji  wakati   utakapowadia.

 

Powered by Blogger.