MSALAKA: ARIDHISHWA NA UJENZI WA SKULI TUMBATU
Na. Mwandishi wetu
Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini 'A', Unguja, Bw. Rashid Simai Msaraka amesema ameridhishwa na maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Tumbatu.
Akizungumza wakati akikagua maendeleo ya mradi huo huko Wilaya Ndogo ya Tumbatu, Bw. Msaraka ameeleza kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia katika hatua nzuri hivyo amewataka Wasimamizi kuzidisha bidii ili waukamilishe Kwa wakati uliopangwa.
Akizungumzia kuhusu miradi mingine inayojengwa katika kisiwa hicho,Bw. Msaraka amesema ujenzi wa miradi ya barabara na afya tayari umeanza, huku mradi wa bandari na uwanja wa mpira unatarajiwa kutekelezwa baada ya muda mfupi.
Post a Comment