WAAFRIKA MIL 300 WATAPIKIA NISHATI YA UMEME IFIKAPO 2030: BITEKO

JUMANNE MAGAZI 

16.10.2024 Dar es salaam 

Naibu Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Dkt Doto Biteko amesema ifikapo mwaka 2030 watu million 300 katika Bara la Afrika wawe wamefikiwa na umeme ili watu wengi waweze kutumia nishati safi ya kupikia.

Ameyasema hayo mapema leo hii alipokua katika uzinduzi wa mkutano wa 9 wa siku 2 wa soko la Nishati Afrika ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati uliofanyika jijini Dar es Salaam katika hotel ya Hayyat

Amesema  juhudi zinazofanyika katika kufikia lengo hilo zimepelekea  Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia ( WB) kuunga mkono Ajenda ya Nishati Safi ya kupikia katika bara la Afrika.

Biteko amesema hayo wakati akizungumza katika Mkutano wa Jukwaa la Majadiliano kuhusu Masuala ya Nishati  kwa Bara la Afrika kwa ngazi ya Mawaziri unaofanyika Jijini Dar es salaam kwa siku mbili ulioandaliwa  na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na AfDB.

Aidha, amesema jambo jengine ni kwamba mkutano huo utakua ni maandalizi ya mkutano wa wakuu wa nchi wa Afrika wanaokwenda kujadili masuala ya nishati kwenye bara la Afrika kwani kuwapata watu 300 sio kazi  rahisi kuishia kwenye ngazi ya Wizara.

Ameongeza kuwa, lengo la mkutano huo ni kwenda kujadili na kufanya tafakuri kubwa kama bara juu ya upatikanaji wa Nishati safi ya kupikia ambapo mfumo wake unachangamoto nyingi kwenye utekelezaji wake.


 Kwa upande wake, Makamo Mwenyekiti wa Nishati, mabadiliko ya tabia nchi na ukuaji wa kijani AFDB Dr Kevin kairuki wameamua kufanya kazi kwa pamoja na Tanzania kwa sababu ipo mstari wa mbele katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

"Tanzania imekua ikitilia manani mambo ya nishati safi ndio sababu tukakaa na wadau kama vile World Benki tukasema hili kongamano lifanyike Tanzania kwani kupata watu million 300 wa kutumia nishati safi ya kupikia sio rahisi" amesema Dr Kairuki.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Eng Felchesmi Mrama amesema mkutano huo wataweza kujadiliana ukuaji wa Nishati, matarajio, namna ya kuipata, uzalishaji na ujumuishaji wa Sekta binafsi kwani ifikapo 2034 wanataka nishati ipatikane kwa unafuu.

Amesema uamuzi wa kuamua mkutano mkubwa wa Marais ufanyike Tanzania ni pamoja na kumuunga mkono Rais Samia katika juhudi za utekelezaji wa Ajenda ya Nishati safi ya kupikia na kuwa kinara wa ajenda hiyo kwa nchi za Afrika. See
Mkutano huo umehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, Kamishna wa Umeme na Nishari Jadidifu Mhandisi Inocent Luoga, Wakuu wa Taasisi zilizochini wa Wizara ya Nishati na wadau wa nishati kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania


masuala ya nishati katika Bara la Afrika ikiwemo suala la  watu milioni 300 Afrika kutumia nishati safi ya kupikia. 
Ameongeza kuwa, mkutano huo utafanya tafakuri na utaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa nishati safi ya kupikia inapatikana kwa uhakika na gharama nafuu ili kila mwananchi anaweza kuimudu.
Amesema mkutano huo ni muhimu kwa Tanzania  hasa kwenye sekta ya nishati kwakuwa imefanya mapinduzi makubwa kwenye nishati  na upatikanaji wa umeme nchini ni wa uhakika na miradi mikubwa inayotekelezwa ipo mwishoni na kwamba kazi kubwa iliyopo ni kuhakikisha watu wanapata umeme kila sehemu



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI


Powered by Blogger.