SINEMA ZETU YAJA NA KITU KIPYA "MIZANI YA MAPENZI" KUANZA KURUKA HEWANI AGOSTI 23

Kampuni ya Azam media ltd kupitia chanel yake ya pendwa ya Sinema zetu Leo hii agosti 12 2024, imetambulisha ujio Rasmi WA tamthiria mpya ijulikanayo kama Mizani ya mapenzi
Mwambulambo amesema Azam tv imewasogezea sebuleni burudani hiyo ya tamthiria ya Mizani ya mapenzi ambayo itakuwa ikionyesha kuanzia Agosti 23 ikichukua nafasi baada ya kumalizika kwa tamthiria ya Toboa tobo ambayo itamalizika Agosti 19 mwaka huu.
Akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa habari mkuu wa maendeleo na maudhui Kutoka Azam media ltd Wasi wasi Mwabulambo  amesema wao kama Azam wameapa kuendelea kutoa burudani kupitia chaneli ya sinema zetu wakiwa na lengo la kutoa burudani kwa WATAZAMAJI wao.

Kwa upande wake  mtunzi na muongozaji  WA tamthiria hiyo bi Davita Richard, amesema wamelenga kutoa Elimu inayohusu mahusiano hususani ndoa na mikasa ya usaliti WA marafiki WA karibu inayojotokeza kwenye jamiii.

Davita ameendelea kufanya kuwa Tamthiria ya MIZANI YA MAPENZI' ni tamthiria iliyojikita Zaidi kuonyesha wanandoa wenye mitazamo tofauti juu ya furaha zao.



 

Powered by Blogger.