HATUTAKUWA NA UPENDELEO WOWOTE KATIKA SEKTA ZA MIUNDOMBINU YA BARABARA MICHEZO,BUYUNI : DIWANI JESCA MSOLLA

Na. Jumanne Magazi

08.06.2026

Dar es salaam.

Diwani wa kata ya Buyuni Mh Jesca Mahamoud Msolla, amesema chini ya uongozi wake hakutakuwa na Upendeleo wowote katika kuwaletea maendeleo au fursa wakazi kata hiyo.

Amesema hayo hii Leo Juni 8,2026 kwenye mahojiano maalumu na mwandishi wetu wakati akifanya majumuisho wa ukarabati wa Barabara ya Taliani Kigezi inayoendelea kwa haya ya msingi (fomesheni).

Msolla amesema "mimi kama muwakilishi wa wananchi wote wakata ya Buyuni ambao walimpigia kura na aliwaahidi kuwaletea maendeleo hivyo sitakuwa na Upendeleo kwani wote ni wananchi wangu"
Amesema kwa sasa ukarabati huo umeanza kwenye Barabara hiyo yenye urefu WA km 4.3 ambayo kwa muda mrefu imekuwa na mashimo na madimbwi Hali inayopelekea usumbufu mkubwa na wamuda mrefu kwa wakazi na watumiaji wa Barabara hiyo.
Wakati huo huo diwani Jesca ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuipa uwezo na fedha halmashari ya jiji kwa ajili ya maendeleo ya kata yake.

Aidha pia Diwani huyo amewashukuru viongozi  wote wa halmashahuri ya jiji la Dar es salaam akiwemo, mkuu WA wilaya,comredi Edward Mpogolo na Mkurugenzi wa jiji  Bw Elihuruma mabelya, kwa kuidhinisha fedha za miradi ya maendeleo kwenye kata yake ya buyuni amesema diwani Jesca msollam

Katika hatua nyingine Msolla amesisitiza kuendelea kufanya kazi usiku na mchana kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi wake ambapo amesema hatoacha kubisha mlango Hadi mlango ikiwe milango hiyo utakuwa Ina fursa za maendeleo chanya kwa kata yake ya buyuni
Aidha ametaja sifa na falsafa yake ya kufanya kazi masaa 24 siku 7 katika juma kitu ambacho amesema kimekuwa kiki pa nguvu na hari ya kufanya mengi makubwa ya kimaendeleo, jambo ambalo amehusia viongozi wengine kufanya kazi KWA maslahi mapana ya wananchi badala ya kujinufaisha wenyewe kisiasa.
 

Powered by Blogger.