JAMII YAASWA KUSAPOTI VIJANA KWENYE MICHEZO KUWAINUA KIUCHUMI: NGATICHE



Na Jumanne magazi 

15.02.2026

Dar es salaam 

Jamii nchini imeaswa,kusaidia vijana wenye vipaji nchini ili kuwainua kiuchumi kipitia vipaji vyao vya michezo. Mbalimbali ikiwemo soka.

Hayo yamesemwa na Diwani wa kata ya kinondoni CCM Idrissa Said Ngatiche, wakati akikabidhi zawadi kwa washindi kwenye bonanza la Adelante lililofanyika Leo jumapili February 15,2026, katika viwanja vya Leaders club kinondoni jijini dar es salaam.

Jumla ya zawadi zenye thamani ya Shilingi mil 1.5, ambapo bingwa wa michuano hiyo, ameibuka na kikombe, seti moja ya jezi medali, na pesa taslimu kiasi Cha Shilingi laki moja.

Aidha Diwani Ngatiche ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana wengine kuepuka kujiingiza kwenye makundi hatarishi na badala yake kutumia michezo kama ajira na fursa ya kujipatia kipatao kupitia vipaji vyao.
Katika hatua nyingine Diwani Idrissa Ngatiche ameiasa jamii kupenda kushiriki michezo kwa lengo la kuhimarisha afya zao,ili kuepuka magonjwa hatarishi yakiwemo Yale yasio ya kuambukizwa

Bonanza hilo limeandaliwa na kamati maalum chini ya ustadh mohd Moshi, likifadhiliwa na Diwani wa kata ya kinondoni MH Idrissa Said Ngatiche pamoja na timu ya Adelante fc yenye maskani yake kinondoni ada estate, jijini dar es salaam, ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka.
 

Powered by Blogger.