KWENYE ELIMU WANA KINONDONI HAWAMDAI RAIS DKT SAMIA: TARIMBA

Na Jumanne Magazi 

Septemba 13 2025

Dar es salaam 

Mgombea mbunge wa Jimbo la Kinondoni 
TARIMBA Abass Gulam, amesema katika 
uongozi miaka mitano ya Rais Dkt Samia 
suluhu hassan amekamilisha MIRADI yote 
ya elimu katika jimbo la Kinondoni.
Ameyasema hayo Leo hii Septemba 13 2025, kwenye mkutano wa uzinduzi wa Kampeni kwa Jimbo la Kinondoni uliofanyika kwenye viwanja vya CCM Mwinyijuma mwanyamala
Awali mgeni rasmi kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa jumuiya ya WAZAZI taifa Mhe Ali salum Hapi amesema chama Cha Mapinduzi kimemteuwa mgombea Abas tarimba kwa kuwa kinatambua mchango na kazi aliyoifanya wakati wa uongozi wake kwenye muhula wake wa kwanza
Tarimba ambaye anawania UBUNGE kwa muhula wa pili amesema amekishukuru  chama Cha Mapinduzi kwa kumuamini na kumteuea kuwa mgombea kwa tiketi ya chama hicho pili ameahidi wananchi wa Jimbo la Kinondoni KUENDELEZA Yale yote waliyoyaanza katika kipindi Cha kwanza
Naye mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM kwa Jimbo la Ukonga mheshimiwa Jerry slaa amewataka wakazi na wananchi wa Kinondoni kumpigia kura mh TARIMBA pamoja na mgombea urais kwa tiketi ya CCM Mhe Dkt Samia suluhu hassan kwenye nafasi ya urais 
Uchaguzi mkuu umepangwa kufanyika Oktoba 29 Mwaka huu ambapo jumla ya vyama 17 vikitataraji kushiriki uchaguzi huo
 

Powered by Blogger.