WAGENI ZAIDI YA 500 DUNIANI KUSHUHUDIA TUZO ZA 32 ZA UTALII KANDA YA AFRICA,DAR ES SALAAM

 Na Jumanne Magazi 

11.06.2025

Dar es salaam 

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Balozi Ephraim Mafuru amewataka wadau wa utalii nchini kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana katika sekta hiyo ikiwemo usafirishaji, huduma za afya, burudani na malazi ili kukuza utalii na kuongeza vipato vyao. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mafuru alisema kuwa sekta ya utalii ina nafasi kubwa katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi endapo wadau wataitumia kikamilifu.

Balozi Mafuru alikuwa akizungumzia maandalizi ya Tuzo za 32 za Utalii wa Kimataifa kwa ukanda wa Afrika na Bahari ya Hindi, zinazotarajiwa kufanyika Juni 28 mwaka huu, tukio ambalo linatarajiwa kuwakutanisha wadau mbalimbali wa utalii kutoka ndani na nje ya nchi. 

Naye Meneja wa Hoteli ya Johari Rotana, Ahmed Said, alieleza kuwa ujio wa wageni kutoka mataifa mbalimbali kupitia tuzo hizo ni fursa adhimu kwa sekta ya hoteli kuonyesha ukarimu wa Kitanzania pamoja na kuitangaza Dar es Salaam na vivutio vyake kama sehemu ya kipekee kwa wageni wanaokuja kwa mapumziko au shughuli za kikazi.

Kwa ujumla, maandalizi ya tuzo hizo yameibua hamasa miongoni mwa wadau wa utalii, huku matarajio yakiwa ni kuinua hadhi ya Tanzania kimataifa kupitia utoaji wa huduma bora na vivutio vyake vya kipekee. Wadau wanaamini kuwa kupitia matukio ya aina hii, Tanzania itazidi kujiimarisha kama kitovu cha utalii barani Afrika.

Naye,Mkurugenzi wa Masoko kutoka hospitali ya Shifaa Victoria Tarimo amesema wamejipanga vyema kuhakikisha wanatoa huduma za kimataifa katika kuwahudumia wageni hao ambao watapata changamoto za kiafya wakati wa tuzo hizo.

Amesema Hospitali imejipanga kusapoti agenda ya Rais Dk Samia ya Tiba utalii kwa vitendo.

Tuzo hizo zilianIshwa mwaka 1993 lengo likiwa kutambua mchango wa wadau walipo katika sekta ya utalii katika maeneo mbalimbali Duniani ambapo sasa zinatarajiwa kufanyika june 26,2025 katika hotel ya Johari rotana  jijini Dar es salaam ambapo hoteli hiyo pamoja na hospitali ya shifaa ndio watakaohudumia watu katika Tuzo hizo inatarajiwa kuwa mwenyeji wa tuzo za 32 za kimataifa za utalii kwa kanda wa Afrika na bahari ya hindi ambapo wageni zaidi ya 500 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki.
Pia,wadau wa sekta ya utalii katika mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kuchangamkia fursa za mkutano huo katika kuwahudumia wageni hao.

Akizungumzia mkutano huo leo june 11,jijini Dar es Salaam Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya utalii (TTB) Ephraim Mafuru amesema lengo la Tuzo hizo ni kutambua mchango wa wadau wa utalii Duniani.

Amesema kuchaguliwa kwa Tanzania kuwe mwenyeji wa Tuzo hizo kwa nchi za Afrika pia kumetokana na ushindi wanchi katika tuzo zilizopita kwani iliongoza kwa kuwa na tuzo 5 tofauti na nchi nyingine za Afrika.

Aidha amwongeza kuwa kampuni mbalimbali zinazojihusisha na utalii zitashiriki ambapo washiriki 38 kutoka sekta bifasi na 12 kutoka Serikalini watashiriki.



 

Powered by Blogger.