NCHI ZA AFRICA ZINAWAJIBU WA KUTAFUTA SULUHU YA MZOZO WA CONGO
Na. Jumanne Magazi
8.7.2024
Dar es salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Samia Suluhu HassanAmesema nchi za EAC na SADC hazipaswi kukaa kimya kwani zina wajibu wa kushughulikia mgogoro huu katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, unaogharimu maisha ya watu wasio na hatia.
Ni muhimu kutafuta suluhisho la kudumu kwa pamoja kama wana jumuiya, kama mtetezi wa amani katika umoja wetu na nchi yangu ya Tanzania itaendelea kusaidia masuala ya kidiplomasia ili kumaliza mgogoro huu.
Rais wa Jamhuri ya Watu wa Kenya, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe. William Samoei Ruto
Mgogoro huu hautaweza kusuluhishwa kwa njia za kijeshi, lazima tukatae kupiga mabomu, ni suluhu za kidiplomasia ndizo zinahitajika kwa kushirikisha wadau mbalimbali. Mtakubaliana nami kuwa mazungumzo ya amani sio udhaifu bali ni kusikilizana na kushauriana.
Hatua za haraka zinahitajika ili kuinusuru DRC na watu wake, hii ni gharama kubwa, tunapaswa tuwaokoe mamilioni ya watu wanaohama kukimbia vita, matishio ya vifo, watoto wanahusishwa katika vikosi vya majeshi, tunahitaji kuchukua hatua kwani usalama wa nchi hiyo unaathiri dunia nzima na athari zake zinatakiwa zisipuuzwe.
Rais wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Emerson Dambudzo Mnangagwa
Katika mkutano huo maazimio yamependekezwa kupelekwa kwenye kamati maalum ambazo zitapitia mapendekezo na maazimio yote ya wakuu hapa ambapo baada ya mwezi mmoja watapleka kwenye mamlaka zingine kuona utekelezwaji wake.
Post a Comment