WANANCHI KUNUFAIKA NA MRADI WA KUZUIA BIASHARA HARAM


Na Saidi Lufune - Dodoma

Wananchi wa Kijiji cha Mlazo na Ndogowe wilayani Chamwino Jijini Dodoma wanatarajiwa kunufaika na Mradi wa  kuzuia na kupambana na biashara haram ya ujangili (IWT) ili kujenga mahusiano mazuri dhidi ya Wanyamapori na  kukuza sekta ya utalii nchini

Hayo yamesemwa  leo Desemba 07, 2024 Jijini Dodoma  na Afisa Wanyamapori Mkuu Bi. Rose Mdendemi wa Idara ya Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii katika  Mafunzo ya kuwajengea uelewa wa pamoja wajumbe wa mradi huo wenye dhana ya kushirikisha  jamii katika uhifadhi Wanyamapori kupitia Jumuiya ya Uhifadhi Wanyamapori 

Amesema lengo kuu la kushirikisha jamii katika uhifadhi ni kutekeleza sera ya Taifa ya Wanyamapori ya Mwaka 2007 inayohimiza Wananchi wanaoishi kwenye ardhi za vijiji vyenye rasilimali za wanyamapori na kuwajibika katika  kuhifadhi rasilimali hizo.

“Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Halmashauri ya Wilaya Chamwino, Jimbo la Mvumi inaendelea na utekelezaji wa ushirikishaji jamii katika  uhifadhi ikiwa ni utekelezaji wa Mradi wa Kupambana na Ujangili na Biashara Haram ya nyara. ” Amesema Bi. Rose

Katika hatua nyingine Bi. Rose amewataka askari Wanyamapori wa vijiji kufuata maadili ya kazi zao na kujenga mahusiano mazuri kati yao na jamii ili kuondoa uadui kati yao Wananchi na Wanyamapori 

“Wizara itaendelea kuwawezesha kwa kuwapatia vitendea kazi kama mahema, pikipiki, kamera na kompyuta, kwahyo endeleeni kufanyakazi kwa ushirikiano na jamii kuhifadhi rasilimali za Wanyamapori ili ziendelee kutusaidia  kupitia mradi huu” Amesema Bi. Rose

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nghambaku Mhe. Harun Siengo ameishukuru  Wizara ya Maliasili na utalii kupitia mradi huo kwa kuwa utasaidia wananchi kutumia fursa zitakazopatikana  kujikwamua kiuchumi na kijamii ikiwemo kupata ajira, kujengewa hospitali na barabara

“Mradi huu utakua chachu ya  maendeleo kwa  wananchi lakini pia kujenga urafiki dhidi ya Wanyamapori kama Tembo, swala na Wanyama wengine  kama walivyoweza kunufaika wananchi wa vijiji vingine tulivyovitembelea” Amesema Mhe. Siengo


Naye Afisa Maliasili na Mazingira wa Wilaya ya Chamwino Bi.Yustina Amo ametoa pongezi kwa wajumbe wa waliohudhuria Mafunzo hayo na kukubali Mradi huo kwakua itakwenda kuondo migogoro kati ya Maafisa wanyamapori jamii za ufugaji na wakulima kwa kujenga urafiki na kukuza shughuli za kutalii katika wilaya hiyo

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa vijiji hivyo wameipongeza serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kutatua migogoro ya wanyamapori na wananchi wa maeneo hayo na kulipwa fidia kwa familia zilizoathiriwa na Tembo katika siku za hivi karibuni

Takribani shilingi billion tatu za kitanzania zimetolewa katika vijiji 230 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kupitia faida zilizotokana na Jumuiya ya Hifadhi za Wanyamapori ikiwa ni jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuipa kipaumbele sekta ya utalii kwa kuutangaza utalii na  kushirikisha   na kukaribisha wafadhili
Powered by Blogger.