TANZANIA KUZINDUA SERA YAKE YA VIWANDA NA BIASHARA

Wizara ya viwanda na Biashara inataraji KUZINDUA sera ya Taifa ya Biashara toleo la mwaka 2023, itakayojulikana na kama National Trade Policy.

Akizungumza mbele ya waandishi WA habari hii Leo Waziri wa Viwanda na Biashara Selemani Jafo amesema sera hiyo inalengo la kuweka mfumo na mikakati madhubuti wenye lengo la kuboresha Mazingira ya Biashara ukienda sambamba na ukuaji WA uchumi endelevu.

Amesema katika uzinduzi huo utafanyika Julai 30 katika ukumbi WA mlimani city uliopo jijini dar es salaam huku Mgeni Rasmi anataraji kuwa Naibu Waziri mkuu na Waziri wa Nishati Mh Dotto mashaka Biteko.

Aidha Jafo amesema washiriki wapatao 300 wanatazamiwa kushirikiana uzinduzi huo ikiwajumuisha wadau mbalimbali Kutoka Taasisi za umma, Taasisi binafsi, mashirika ya Dini, wabia wa maendeleo, mabalozi,vyama vya wafanyabiashara na wenye viwanda na Biashara.


Aidha Waziri jafo amesema historia inaonyesha Baada ya Tanzania kupata Uhuru 1961, Shughuli zote za uchumi ikiwemo Biashara ziliendeshwa kwa kiasi kikubwa na Sekta Binafsi. 

Lakini baada ya Azimio la Arusha mwaka 196, Shughuli za uchumi ikiwemo Biashara za jumla mauzo ya Nje ya nchi pamoja na uagizaji WA bidhaa ziliendeshwa na Taasisi za Umma.

Vilevile Waziri Jafo hakuacha kuzungumzia mafanikio yaliyopatikana kupitia Utekelezwaji WA sera ya Taifa ya Biashara ya mwaka 2003.

Vilevile Waziri Jafo hakuacha kuzungumzia mafanikio yaliyopatikana kupitia Utekelezwaji WA sera ya Taifa ya Biashara ya mwaka 2003.

Ambapo amesema Serikali umefanikiwa kushiriki kikamilifu katika majadiliano mbalimbali ya Biashara baina ya nchi na Nchi.

Ikiwa sambamba na jumuiya mbalimbali za kikanda pamoja na kupata fursa za biashara kwenye Kanda hizo ambapo amezitaja baadhi ya Kanda hizo zikiwemo EAC,SADC,AFCFTA, pamoja na masoko mbalimbali ya biashara Kutoka Nchini China

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Trade Mark Africa Bw Elibariki Shammy ameipongeza Wizara ya viwanda na Biashara kwa hatua, hiyo kubwa ya kuzindua sera ya Taifa ya Viwanda na Biashara kwani huo ni muelekeo mzuri kwa. Taifa katika kukupa kiuchumi, pamoja na kuweka Mazingira Bora kwa wawakezaji katika  Sekta ya Viwanda na biashara hapa Nchini.
 

Powered by Blogger.